Header Ads

Breaking News
recent

Corinthians yaongeza dau kwa TEVES

Klabu ya soka ya nchini Brazil, Corinthians, imeongeza pesa itakazotoa katika juhudi za kumsajili nahodha wa Manchester City, Carlos Tevez. 

Mapema Corinthians walitaka kumnunua Tevez, kutoka Argentina, kwa pauni milioni 35, lakini inafahamika sasa wameongeza kitita hicho hadi pauni milioni 39.

"Ninafahamu wameongeza pesa", wakala wa Tevez, Kia Joorabchian aliielezea BBC, "lakini ombi hilo liliwasilishwa Ijumaa, na hizi ni hatua za mwanzo tu."

Carlos Tevez


Anataka kukaribia nyumbani Argentina

City wana nia ya kumuuza Tevez kwa pauni milioni 50.

Hawataki kuharakishwa kuafikia makubaliano upesi, lakini meneja Roberto Mancini atapata nafasi bora zaidi katika kumtafuta mchezaji wa Atletico Madrid ya Uhispania, Sergio Aguero.

City wanahisi hawajapungukiwa kifedha, na kwa hiyo hawana shinikizo katika kumuuza Tevez, ambaye pia ana mkataba mrefu, na inaaminika ni zaidi ya pauni lakini mbili kwa wiki.

Kwa hiyo ahadi za Corinthians huenda zikakosa kuivutia Manchester City katika kumuuza Tevez, mwenye umri wa miaka 27, na aliyeisaidia klabu katika kulipata kombe la FA, na timu kufuzu kuingia ligi ya klabu bingwa barani Ulaya.

Kuhamia Marekani Kusini ni jambo ambalo litamsaidia Tevez katika kuikaribia zaidi familia yake.

Iwapo ataondoka, raia mwenzake wa Argentina, Aguero, na mwenye umri wa miaka 23, na ambaye huichezea Atletico, anatazamiwa kujaza pengo litakaloachwa na Tevez.

Lakini City hawataki kufanya juhudi hizo kabla ya kuwa na uhakika ikiwa Tevez ataondoka au la.

No comments:

Powered by Blogger.