ESSIEN APASULIWA GOTI
Kiungo wa klabu ya Chelsea Michael Essien hatacheza soka kwa muda wa miezi sita baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti.

Michael Essien
Meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas ameeleza katika mtandao wa klabu hiyo: "Kila mmoja anamtakia Michael apone haraka.
"Wachezaji wenzake na wafanyakazi wote pamoja na mimi tupo tayari kumsaidia aweze kurejea uwanjani haraka iwezekanavyo."
Mwaka 2008 Essien hakucheza soka kwa muda wa zaidi ya miezi sita baada ya kuumia goti.
Pia hakuweza kuiwakilisha Ghana katika mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 2010 kwa sababu ya matatizo hayo hayo ya goti.
No comments: