Nana Rawlings wa Ghana ashindwa Urais

Bi Nana Rawlings
Nana Konadu Rawlings alishinda kwa asilimia 3.1 tu ya kura zote, katika mkutano wa chama cha National Democratic Congress (NDC) kwenye mji mkuu, Accra.
Chama hicho kimeidhinisha Rais John Atta Mills ndiye agombee.
Wachambuzi wamesema kugombea kwa Bi Rawlings kumeonyesha nia ya mumewe ya kuwa na ushawishi zaidi katika chama hicho.
Wakati wa kamepni, Bi Nana alisema alikuwa akimpa changamoto Bw Atta Mills "kuiokoa" NDC.
No comments: