Header Ads

Breaking News
recent


                   WAZUNGU  wawili wenye asili  ya uingereza walikamatwa na nyara za serikali.



Tukio hilo lilitokea mnamo tarehe  30 june mwaka huu wakati askari wa idara ya uhamiaji  wilayani humo wakiwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Walifanikiwa kuwakamata   NICHOLAUS VIDMR. Na HOUS CHABERS,Wakiwa na nyara za serikali pembe nne za tembo,

Waingereza hao walifikishwa mahakamani  jana tarehe 8 Julai mwaka huu katika  mahakama ya hakimu mfawidhi  Mkoa wa  Mbeya.

Mwendesha mashitaka wa polisi GRIFFIN MWAKAPEJE.  Aliwasomea  shitaka hilo mbele ya  hakimu mfawidhi wa mkoa wa Mbeya ZABIBU  MPANGULE.

Washitakiwa hao hawakutakiwa kujibu lolote kutokana na kosa hilo ambalo ni uhujumu uchumi, washitakiwa wote walipelekwa rumande hadi tarehe 21 julai mwaka huu itakapotajwa tena.
 
Wakati huo huo Jeshi la Polisi Mkoani Imeanzisha msako kwa watu waliohusika kumuua Mwalimu JUMA said.

Akizungumza Waandishi wa Habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi alisema JUMA SAID (56) aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi Utengule aliuwa na watu awasiojulikana Julai 7 saa 2.33 usiku akiwa nyumbani kwake utengule Mbalali Kamanda Nyombi alisema marehemu ambayepia alikuwa mfanyabiashara.

''Baada ya kuvamiwa na majambazi alapigwa risasi mbili kwenye paja kabla ya kuporwa pesa ambazo hazikujulikana thamani yake, Msako mkali na tunaomba ushirikiano kutoka kwa wananchi,alisema Kamanda  Nyombi.

No comments:

Powered by Blogger.